Description
Mzee Tamaa alisikia sauti ya Mwalimu Rose. Alitoka alikokuwa ameketi na kuwakaribia Ruto na Mwalimu Rose.
“Wewe ni nani na unafanya nini hapa kwangu?”Mzee Tamaa alimuuliza Mwalimu Rose kwa ukali.
“Naitwa Mwalimu Rose na Ruto ni mwanafunzi wangu,” Mwalimu Rose alijibu kwa upole.
Je, Ruto atapata haki?





