Description
Sudi ni mvulana aliye na sifa za kiajabuajabu tangu anapozaliwa.Anazaliwa usiku wa manane,anatabasamu na ana sura jamali.Anapoanza kukua,anawashangaza wazazi na ndugu zake kwa jinsi anavyoelewa na kufanya mambo kwa haraka tofauti na watoto wengine.Vitendo vya Sudi pia vinawashangaza wanakijiji.Mambo mengi anayoyafanya Sudi yanafanya watu kuamini kuwa yeye si mvulana wa kawaida.Je, ni mambo yapi anayoyafanya Sudi na yanayowashangaza wengi?





