Description
Tulichea mwajificho hadi tukachoka tiki! Tuliketi hapo penye shina la mbuyu ili tupumzike kabla yakufumukana.
Nilisikia sauti za cha! Cha! Cha! Niliangalia juu zilikotoka.Matagaa ya mbuyu yalikuwa yametanzana. Yalikua meusi tititi.Ghafla, nilimwona nyoka mkubwa akinyiririka kutoka kwenye tagaa moja.Alikuwa akiteremka, kuja mahali tulipoketi.
“Jamani! Nyoka mkubwa anatujia!” nilipiga ukelele….





